Soka linakaribia kurudi baada ya kusimaa kwa wiki kadhaa sasa kutokana na kusambaa kwa ugonjwa wa viirusi vya Corona.
Katika bara ya Ulaya Ujerumani ndiyo inayoonekana kuwa mbele kuliko nchi zote kwani tayari timu nyingi za kijerumani zimeshaanza mazoezi na tayari ratiba mpya imeshatoka ambapo ligi hiyo itaanza tena jumamosi ijayo.
Uingeleza ambayo imeadhirika zaidi kwa virusi kuliko Ujerumani na Hispania, wao watapiga kura jumatatu ijayo na kuamua tarehe ya kuanza tena kwa ligi hiyo.
Ufaransa wao waliamua kuifuta ligi ya mwaka huu na kuamua kuwazawadia PSG ubingwa wa ligi licha ya kwamba ligi ilikuwa bado haijamalizika.
Wiki hii kumekuwa na maendeleo mazuri kuhusu kuanza tena kwa ligi kuu ya Hispania kwani timu nyingi tayari ziemashaanza kufanya mazoezi.
Moja ya timu za Hispania zilizoanza mazoezi ni Barcelona ambapo wachezaji wake wengi walionekana katika viwanja vya mazoezi wa Barcelona ‘Camp Titanova’ wakifanyiwa vipimo vya afya kabla ya kuanza mazoezi.
Kwa upande wa Arsenal bado timu haijaanza rasmi mazoezi ingawa viwanja vya mazoezi vya Arsenal vilifunguliwa zaidi ya siku 10 zilizopita ambapo wachezaji wanaruhisiwa kufanya mazoezi peke yao.
Hapo chini ni video ya timu ya Barcelona wakiingia katika viwanja vyao vya mazoezi.