Mchezaji wa kiungo wa Arsenal Henrikh Mkhitaryan, amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa Arsenal kwa mwezi wa pili.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Armenia amekuwa akicheza vizuri tangu apone majeraha yaliyomfanya akose mechi za mwisho wa mwaka jana na mwanzoni mwa mwaka huu.
Alikuwa katika kiwango bora mwezi wa pili baada ya kumtengenezea goli Alexander Lacazette kabla ya kufunga dakika 10 baadaye katika mchezo dhidi ya Southampton.
Mkhitaryan pia alifanya vizuri katika mchezo dhidi ya Bournemouth, baada ya kumalizia pasi aliyopigiwa na Mesut