Jana ilikuwa ni siku ya kiishoria baada ya kurudi soka la ushinda kutokana na kusimama kwa wiki kadhaa baada ya kuibuka kwa virusi vya Korona.
Ligi kuu ya Ujerumani maarufu kama Bundersliga jana ilikuwa ya kwanza kuruhusu michezo ya ligi kuu kuendelea baada ya kusimama kwa muda.
Kutokana na kutokuangaliza mchezo wa soka kwa muda mrefu, mamilioni ya mashabiki wa soko duniani kote walikuwa na shauku wa kuona nini ambacho kingetokea.
Kuna mambo mengi yaliyotokea lakini kwangu mimi haya matatu ndiyo yaliyonifanya nione tofauti kubwa na kabla ya ugonjwa huu.
Hakukuwa na msisimuka kabla ya mchezo
Tumeshazoea kuona mashabiki wakimiminika uwanjani masaa machache kabla ya mchezo na pia saa moja kabla ya mchezo timu kuanza kupasha na kuibua hamasa kubwa, katika michezo ya jana na leo hicho kitu hakikuwepo, viwanja vilikuwa kimya na wachezaji walipotoka kupasha walikuwa wanaonekana kama maninja na si wachezaji wa soka.
Nimesikia sauti ambazo si kawaida kuzisikia
Naandika haya ikiwa ni mapumziko katika mchezo kati ya Bayern Munich na Hertha Berlin, katika kipindi cha kwanza mchezaji wa Bayern alianguka na ulikuwa unaweza kusikia mtu akipumua na pia unasikia baadhi ya sauti kutoka benchi la ufundi, hivi ni vitu ambavyo kwa kawaida hatujazoea kusikia ama kuona.
Ushangiliaji wa magoli umebadilika
Jana niliona Borrussia Dortmund walivyoshangilia magoli yao, walikuwa wakishangilia wakiwa umbali wa kama mita moja kutoka baina yao.
Leo nimeona Bayern Munich wakishangilia goli ya Lewandolski kwa kupigana vikodo ni aina ya ushangiliaji ambao hatujauzoea lakini ilikuwa vizuri kuona.
Kilichonifurahisha
Pamoja na kuwa na vitu vingi ambavyo si kawaida kuviona katika soka, kilichonifurahisha kwa kweli ni kiwango cha uchezaji, michezo yote niliyoiona ilikuwa katika kiwango cha hali ya juu.
Pia baada ya mchezo kuanza ukielekeza mawazo yako katika kutazama soka hutagundua ya kwamba hakuna mashabiki kwani katika spika za wiwanjani kuliwekwa nyimbo ambazo mara nyingi mashabiki huziimba viwanjani.
Pamoja na hayo kuna baadhi ya wachezaji hawakuwa fiti, asilimia kubwa ya wachezaji wa Shalke 04 walionekana kuchoka mapema ndiyo maana walipigwa 4-0, huku Dortmund wakionekana kuwa fiti zaidi ukiondoa Jordan Sancho aliyeonekana kukusa mazoezi na pia kama ameongezeka uzito.
Nategemea Arteta atakuwa ameona hilo kwani ligi kuu ya Uingeleza ikirudi na timu ikiwa haipo fiti itakuwa ni ngumu kupata ushindi.
Tarari kipindi cha pili kinaanza hapa acha niendelee akuangalia soka, jumapili njema.